Friday, November 30, 2012

SMZ yazuia wananchi kushuhudia kesi ya Uamsho,

Katika kile kinachoonekana haki kutolutendeka na vyombo vya dola kushindwa kuhedhimu muhimili wa mahakama, SMZ leo imeendeleza ubabe wake na kuvunja uhuru na taratibu za mahakama katika mashitaka y dhidi ya wanaharakati na viongozi wa UAMSHO
Viongozi saba wa Jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho walifikishwa katika Mahakama Kuu ya Vuga mjini Zanzibar hivi leo, lakini chini ya ulinzi mkali wa karibuni vyombo vyote ya ulinzi na usalama, huku wananchi wakizuiwa kabisa kukaribia hata eneo la mahakama hiyo.
Askari wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, wakiwemo wale wa Jeshi la Kujenga la Taifa (JKU), waliyazingira maeneo yote yanayokaribianana jengo la Mahakama Kuu, huku wakiwazuia watu hata kukaribia jengo hilo. Watu wengi walioachangia maoni yao kupitia mitandao ya kijamii kuhusu namna kesi hii inavyoendeshwa,­wamesema kwamba usiri, nguvu na vitisho vya hali ya juu vinavyooneshwa na SMZ katika muendelezo wa kesi hii, vinaashiria ukosefu wa uadilifu, woga na kutokujiamini kwa serikali mbele ya viongozi hao wa Uamsho iliowakamata.
"Hao (askari wa SMZ) hawana kazi za kufanya ndio maana wameambiwa nendeni mkakusanyike alau muonekane kama mpo. Na hiyo ni ushahidi kuwa hao Uamsho wana nguvu kuliko hao wanaoiendesha hiyo kesi….", yalisomeka maoni ya mchangiaji mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Dula Said.
Mchangiaji mwengine aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Abbas Machano alisema kwamba binafsi alipita karibu na eneo la mahakama na akaona kwamba "mpaka njia ya kwendea Mnazi Mmoja imefungwa", akiongeza kwamba hilo halikuwa jambo la haki kwani "watu wanahitaji kupata taarifa."
Awaali mawakili wa viongozi hao walikuwa wamelalamikia kuwepo kwa jaji asiyeweza kutoa dhamana kwa watuhumiwa hao na hivyo wakawasilisha madai yao ya kubadilishiwa jaji mwenye uwezo wa kutoa maamuzi. Itakumbukwa kwamba tangu viongozi hao walipokamatwa kwa mara ya kwanza zaidi ya mwezi mmoja sasa, bado hawajapatiwa dhamana, licha ya dhamana zao kuwekwa wazi, lakini kwa masharti ambayo wengi wanaamini kwamba ni sawa na kulazimisha waendelee kubakia rumande wakati kesi yao ikiendelea kusikilizwa.
Kutokana na maombi ya mawakili hao, wamefanikiwa kuweza kubadilishiwa jaji ambae atakuwa na uwezo kwa kuitolea maamuzi kesi hiyo. Lakini katika tukio la leo, Jaji huyo aliweza tu kuwaita kwa majina yao na kisha kuahirisha tena kesi hiyo hadi tarehe 6 Disemba 2012.
Inshallah



No comments:

Post a Comment