Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma, leo wamehudhuria msiba wa baba yake na muigizaji wa filamu nchini Wema Sepetu, Balozi Abraham Sepetu aliyefariki jana baada ya kuugua kwa muda mrefu maradhi ya kisukari na kiharusi. Alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam..
Balozi Sepetu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje mnamo miaka ya 1970 wakati wa utawala wa awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Julius KambaragE Nyerere.
Vilevile, aliwahi kuwa balozi nchini Urusi tangu mwaka 1982 wakati wa utawala huohuo wa Nyerere. Hadi anafariki, Mzee Sepetu alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.
No comments:
Post a Comment